Kuwa chini ya sheria ni sawa na kuwa na simu “feki” ambayo kila wakati unahofu kuwa TCRA wataizima
June 21, 2016 § Leave a comment
Kuwa chini ya sheria ni sawa na kuwa na simu “feki” ambayo kila wakati unahofu kuwa TCRA wataizima. Kuishi katika neema ya Kristo ni sawa na kuwa na simu “original” hata siku ya kuzima simu feki wewe hutaona chochote katika simu yako. Utakuwa unaendelea ku-whatsapp kama kawaida!
Katika neno la Mungu Mtume Paulo kazungumza changamoto za kuishi maisha ya utii na kusema wazi kuwa tukimwamini Kristo hatuko chini ya sheria. Kuna watu huwa hawaelewi wanafikiria kutokuwa chini ya sheria basi ni kuvunja sheria na kutokuwa waangalifu wa kufuata taratibu iwe za kiroho (moral laws – Amri kumi za Mungu Kutoka 20:1-17 ambazo zimegawika sehemu mbili ya kwanza: Amri ya 1 – 4 Upendo kwa Mungu aliyetuumba na sehemu ya pili Amri ya 5 – 10 Upendo na mahusiano na binadamu wenzetu), kimwili kama sheria za afya (health principles) au sheria za nchi (civil laws). Dhamira ya hatia hutusumbua kwa sababu ya kuvunja sheria au kuishi kinyume na taratibu na kanuni. Kuondokana na hiyo ni bora kumwamini Yesu na kumtegemea maana yeye husamehe makosa na kuyafuta kisha hutuwezesha sasa kuishi ndani ya utii.
Leo nizumguzie sehemu ya sheria za afya. Wengi leo tuna madhira makubwa kimwili kwa sababu ya kutokuheshimu sheria za afya. Mfano ulaji (tule nini), Unywaji (tunywe nini), Hewa (tuvute hewa yanamna gani) na kadhalika. Kuna baadhi yetu tumegeuza miili yetu kuwa madampo. Tunapakiza kila aina ya uchungu ndani ya miili yetu. Katika kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 11, Mungu aliwapa wanadamu sheria za ulaji. Ujue binadamu wa mwanzo walikuwa hawali nyama. imekuja kuruhusiwa baada ya gharika. Hata hivyo Mungu aliweka utaratibu wanyama wapi wa kuliwa na wapi si wakuliwa. Tuache ubishi. Tena tukiweza tuache tu kula nyama maana haikuwa katika mpango wa Mungu Tangu alipotuumba.
Sigara, mirungi, madawa ya kulevya, bangi, pombe na jamii yake tutafakari na kufanyia mazoezi ya kuacha kutumi vitu hivyo vina madhara makubwa si katika afya zetu tu bali hata kwa afya ya familia na jamii kwa ujumla. Kuna ubishi mwingi na sarakasi kwenye haya lakini uchaguzi wa kuacha ni salama kwetu. Kuna kijitabu nilikisoma zamani, kinaitwa, “Watumwa Wangali hata Leo”. Kinasema utumwa si tu ule wa zamani au kikoloni. Kuwa mfungwa wa kutumia vitu (addiction) ni ka aina ka utumwa kabaya sana. Kuna watu wanahangaika kutoka kwenye utumwa huu, wana nia ya kuacha lakini imeshindikana. Niwape matumaini kuwa inawezekana. Mzee mmoja rafiki yangu ni raia wa nchi fulani ambapo uvutaji wa sigara umetamalaki kupita maelezo. Nikajaribu kumuuliza kama anajua madhara ya sigara, akasema anayajua na ilishamharibu koo akafanyiwa upasuaji. Lakini akaniambia ndiyo starehe ilyobaki hawezi kuacha mpaka kufa. Huyu ni tofauti na wengi wengine wetu. Wengi hawajui madhara ya sigareti. Tumeweka utaratibu katika matangazo ya sigara kwamba ina madhara kwa afya yako. Maandishi haya hayaeleweki maana yake nini hasa kwa watumiaji. Tataendelea kuweka msukumo kwa viwanda hivi hatari vifungwe kuokoa maisha ya watu wetu.
Ulaji wa mbovu: unaweza kuwa unakula kuzingatia kanuni za nini ule lakini hufuati utaratibu mzuri wa kula. Hii nayo ni hatari. Kuna watu wanakula ovyo ovyo. Akiona kitu hata barabarani udenda unamtoka. Kanywa chai, Kala mchana na hata usiku. Lakini anataka ale pia katikati, akiona tukaranga huyo, korosho hazimpiti, Vitumbua anavyo, maandazi ooohhhh!, Juice za Azam barabarani hazikatishi mbele yake. Mikia ya pweza yumo. Akiona mtu anapitisha tumhogo atataka hata kakipande kadogo tu. Keki hazipiti, sijui aiskrim, popcorn, tuvikombe twa kahawa barabarani na vingine vingi, havikatishi mbele ya macho yake. Hii ni hatari. Kwanza unaweza kula vitu ambavyo haviko katika usafi (ukaambukizwa magonjwa), pia tumbo linahitaji muda wa kusaga chakula ulichokula ama asubuhi au mchana au jioni. Tujiepushe na kula katikati ya milo. Tuna shida ya mila na desturi pia, mtu akija kwako akikwambia kashiba usimlazimishe eti akuachie baraka – yeye unamwachia laana. Tunywe maji ya kutosha (walau lita mbili) kwa siku. Kuna watu asubuhi hadi jioni hanywi maji halafu anajisifia ka zuzu, “mie naweza kwenda hata siku mbili bila kunywa maji”, ole wako. Kunywa maji nusu saa kabla au baada ya kula, usinywe maji huku unakula chakula unaharibu na kuchelewesha mfumo wa kusaga chakula.
Chakula kiwe kamili (balanced diet) vyakula vya kukinga mwili, kuleta joto na kujenga mwili. Usikoboe nafaka mfano mahindi. Yasage hivyo hivyo. Kwa nini uzidiwe akili na wadudu na panya? Wakila mahindi wao hula kiini cha hindi. Maganda yanayozunguka hindi ni ufagio tumboni mwako. Kula vyakula vyenye jamii ya mifagio mfano mboga za majani nyingi. Usione ufahari kukaa muda mrefu bila kwenda haja kubwa. Hiyo ni hatari!
Leo niishie hapa kwa afya: Tukitii kanuni za afya itakuwa sawa na kuwa na simu original wewe utayeya tu na mawasiliano. Ukiendekeza kuvunja kanuni za afya utakatwa kama yule jamaa yangu.
Je, mitambo ya kusindika vyakula Tanzania inatumia “food grade lubricants”?
March 6, 2016 § 2 Comments
Jana nilikuwa na rafiki yangu anayehusika na mambo ya viwango tukazungumza mambo kadhaa kuhusu viwango vya bidhaa mbalimbali hapa nchini. Kuna wakati niliwahi kurusha kwenye mtandao mwingine juu ubora wa nondo tunazojengea hapa nchini baada ya kuzifanyia majaribio binafsi. Bahati mbaya kabisa viongozi wetu wa mashirika kama TBS au taasisi kwa ujumla ama hawako au hawashiriki kwa mitandao ya jamii. Nashauri wafanye hivyo ili tusaidiane na umma kuibua matatizo ya viwango.
Tanzania tuna viwanda vya kusindika vyakula na madawa kwa ajili ya matumizi ya wanadamu na mifugo ambayo wengi wetu huila pia au kutumia mazao yake kama maziwa nk. Tukiwa na mjadala na huyu ndg yangu nikaibua hoja ya vilainishi vya mitambo inayosindika vyakula. Katika mitambo hiyo Kuna sehemu tunaita nyeti (critical areas) ambapo chakula kinaweza kutana na vilainishi kiuhalisia kulinda afya ya binadamu nchi zilizoendelea zimeamua tu kwamba mtambo unaosindika vyakula wote ni critical. Hivyo ni lazima kutumia “food grade lubricants” mazao ya plastic zinazotumika kubeba chakula na maji ni lazima ziwe food grade pia.
Sasa swali: je, viwanda vyetu vinavyozalisha chakula vinatumia food grade lubricants kuepusha uchafuzi wa chakula? Nani anahakikisha hilo linafanyika? Total food grade policy Inatokana na ukweli kwamba mafundi wanaweza kuchanganganya lubricants hivyo kuondoa huo uwezekano ni kutumia food grades kwa mitambo yote ya kusindika vyakula. Na watu wasitoe sababu, kwenye soko tuna hydraulic oil, transmission oil, greases za food grade.
Tujilinde wapendwa na wenye mandate hiyo ni TBS na TFDA.
Wanaume tulofikisha miaka 40 tupime tezi dume tuache kujazana ujinga
January 30, 2016 § Leave a comment
Nimeona watu wanafanya mzaha juu njia ya kupima ukuaji wa tezi dume iitwayo DRE (Digital Rectal Examination) Tukumbumbuke tu kwamba si kila kukua Kwa tezi dume ni kansa. Kuna ile madaktari wanaita Benign Prostate Hyperplasia. Kuna dawa ya ku-control kwa sababu ikikua huminya kibofu Na kufanya uende haja ndogo mara Kwa mara. Niwasihi sana wanaume tuache myths za kijinga Na uoga usio Na maana. Matatizo ya tezi dume yakigundulika mapema hutibika. Kama mtu kafikisha miaka 40 Ni muhimu akapime na baada ya hapo daktari atakushauri uwe unapima kila baada ya muda gani.
Kuna njia tatu ninazozifahamu Za kupima tezi dume, tuzipitie kama nilivyozinukuu:
1. PSA blood test (nimeshafanya kipimo hiki ikiambatana Na cha ultrasound)
Maelezo kutoka UK Cancer research test ni Haya:
PSA is a protein produced by both normal and cancerous prostate cells. A high level of PSA can be a sign of cancer. But your PSA level can also be raised in prostate conditions that are not cancer (are benign) or if you have an infection. To check for PSA (prostate specific antigen), your doctor takes a sample of your blood. Your doctor may want to rule out a urine infection before carrying out a test. If you’ve had a urine infection, you shouldn’t have a PSA test for at least a month after your treatment finishes.
PSA is usually measured in nanograms per millilitre of blood (ng/ml). There is no one PSA reading that is considered normal. The reading varies from man to man and the normal level increases as you get older. But the following values are a rough guide
3 ng/ml or less is considered to be in the normal range for a man under 60 years old
4 ng/ml or less is normal for a man aged 60 to 69
5 ng/ml or less is normal if you are aged over 70.
A reading higher than these values but less than 10 ng/ml is usually due to a non cancerous (benign) enlargement of the prostate gland. A reading higher than 10 ng/ml may also be caused by benign prostate disease, but the higher the level of PSA, the more likely it is to be cancer. Sometimes a cancer may be diagnosed in a man with a PSA reading within the normal range. But usually, the higher the reading, the more likely it is to be cancer.
Some men have PSA levels in the hundreds (or even thousands) when they are diagnosed. The higher the level of PSA at diagnosis, the more likely the cancer is to spread quickly.
PSA blood tests are also used to monitor how well prostate cancer treatment works or to decide whether you need treatment. If your PSA is stable, it is a sign that a cancer is not growing or spreading. Successful treatment shrinks cancer and so the PSA level in the blood then falls.
2. Rectal examination (nadhani ndo wanaume tunachokiogopa)
Maelezo yake kutoka chanzo kilekile Ni Haya:
Your doctor puts a gloved finger into your back passage (rectum) to feel your prostate gland and check for abnormal signs, such as a lumpy, hard prostate. Doctors call this test a digital rectal examination (DRE).
Mchoro unaonyesha tezi dume ilipo nimeambatanisha. Ukiangalia huo mchoro uatajua Kwa nini madaktari hutumia njia hii ya DRE (Digital Rectal Examination) kupima.
3. Rectal ultrasound (hii hasa ni kuchunguza tezi dume kitu Kama ukubwa wake)
You may have a rectal ultrasound scan to examine the prostate gland. It is called a trans rectal ultrasound (TRUS). You will need to make sure you have had a bowel movement beforehand so that your rectum is empty when you go for your appointment.
Your doctor puts a small ultrasound device into your back passage. It produces sound waves to create a clear picture of the prostate gland. This test is uncomfortable, but shouldn’t hurt. It does not take long.
Illness is part of Over 71% of Dar residents’ life
July 16, 2012 § Leave a comment
Confirming the findings of the previous two Listening to Dar health reports, the study has revealed that for many citizens of Dar es Salaam, illness is very much part of everyday life. In the current survey recently released by Listening Dar, 71.3% of respondents report a case of illness in their household during the four weeks prior to the interview.
This and other findings concerning state of health services in public facilities you can find in the report below. Lack of medicines and preferential groups not receiving medical services as provided for by the Health policy are common occurrences in Dar es es salaam health facilities. If this is happening in the commercial and de-facto capital city of Tanzania, what about health facilities far beyond Dar es salaam. As citizens what shall we do about this?
Has the government failed or citizens have failed. Who is to hold the other accountable? Should it be the tax payer or the Tax collector? Reader you have all the answers.
Dr. Ulimboka’s episode: Perhaps this could shed some light to what happened
July 9, 2012 § Leave a comment
Below (doctors) is a letter written to UN asking for among other things Dr. Ulimboka’s protection, he is currently admitted at some unknown location in South Africa. As the letter speaks the threat is so high that other Doctors feel unsafe too. Tanzania has been a very peaceful country for quite sometime now but of recent things are changing and perhaps it doesn’t feel safe anymore.
Have we really exhausted the stock of peaceful means to resolve Doctors’ issues. When we are sick we fully and wholly entrust our lives to Doctors, some procedures they perform to us require sedation, we lay unconscious into their hands. We became like innocent newborn baby but yet they strive with their utmost skills to bring us to conscious again. They are demanding better working environment not only for them but also for us. Yes we may disagree on the methods they are using to press for their demands but (if at all this proves to be the case) brutalizing and intimidating them doesn’t in iota measure compare to what this profession does for our lives.
Thanks to Maria for sharing this.