Ni wakati wa kutafakari na kufanya maamuzi sahihi: Kwa miaka 38 tumekuwa nchi ya kauli mbiu kila baada ya miaka 5

September 25, 2015 § Leave a comment

Ethiopia wamezindua treni ya umeme ninachojua ni ya kwanza kwa East, central Africa na Southern Africa (ukitoa South AFrica) (sijui West na North Africa kama wana treni ya namna hiyo) Nilikuwa Ethiopia mara ya kwanza mwaka 2003 na mara ya mwisho mwaka 2009. 2009 nilikuta wamemaliza:

– kujenga ile ring road na sasa hivi treni ya umeme!

– Njaa iliyokuwa inatesa nchi ni historia!

– Kahawa wanaongoza sasa!

– Viwanda vidogo vimeshakua na vinazalisha kwa masoko ya nje
pia mfano viatu!

– Shirika lao la ndege ni kubwa kuliko mashirika yote ya ndege
Africa!

– Kazi ya kujenga bwawa kubwa la Hidase la kuzalisha umeme wa MW 6,000
litakalokuwa la 11 kwa ukubwa duniani na linajengwa kwa fedha za ndani,
ujenzi umefikia kiwango cha zaidi ya %50 sasa! n.k

Hiyo ndiyo tofauti kati ya inchi inayoongozwa na watu wa vitendo na nchi inayoongozwa na watu wa longolongo. Kama raia wa nchi hii nina siku kadhaa za kufikiria na kuamua. Ili tusonge inaonekana itabidi tuachane na upenzi huu tulete mabadiliko na siyo marekebisho tu. Logic inaanza kunituma kuwa huwezi kulisukuma gari bovu ukiwa ndani, ni lazima utoke nje. Inaonekana tarehe 25 October mwaka huu nitashauri Watanzania wote bila kujali itikadi tulizokuwa nazo na upenzi tutoke kwenye hili gari tulisukume. Ninampenda sana Dr Magufuli lakini naipenda zaidi nchi yangu. Tunataka sasa Tanzania nyingine ambayo viongozi tuliowapa dhamana kila kukicha watakuwa wanatafuta sababu kwa nini jambo fulani lisifanyike na si kutumia muda na mali zetu kutafuta sababu za kuelezea kwenye majukwaa kwa nini halikufanyika.

Mungu ibariki Tanzania!

Mungu ibariki Africa

Where Am I?

You are currently viewing the archives for September, 2015 at kadulyu.