Zitto and Chadema leadership failed to capitalize on the dividends of the law of concentration in politics

March 10, 2015 § Leave a comment

Not sure whether what I’ve read on social networks is true, that Zitto Kabwe’s case against his party (Chadema) has been quashed by the high court I read this from (http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/2648340/-/s4qsn7z/-/index.html) this afternoon. Mwananchi is a credible media house, let us give it the benefit of doubt. This will cast a controversial landscape in our politics and a transient of events at this critical time, especially complicated by the fact that after successful delivery on #TegetaEscrow scandle I was expecting Zitto and Chadema to quickly iron out their differences.
Many of us have different views on this matter perhaps we wait and see what this will lead up to. I have a strong conviction that leaders can sometime subdue their interests for the sake of national interest. To me I think both Zitto on one side and Chadema on the other have failed us. What would be of utmost importance for the alternative political force in Tanzania was to ensure they steer up the second liberation of our country, whatever follows thereafter is trivial and can be suppressed for this grand purpose. Take an example of South Africa, I know there were other heroes more than Mandela who relatively paid the same price as him. Yet these guys (the leaders of anti-apartheid movement) were focussed. They all decided to unite and agreed to symbolize their resistance through Madiba. Madiba became the epicenter of change where all all energies were concentrated upon. It doesn’t mean that there were no other political prisoners in South Africa, there were many but people like Oliver Tambo and the rest realized the importance of THE LAW OF CONCENTRATION and fully capitalized on it. It finally paid its dividend. Opposition leaders in Tanzania need to understand this law too and use it to the advantage of the citizens of Tanzania.
There is no dispute that Zitto is a formidable politician, he is effective in addressing and dealing with the menaces of the political creed. He carries with him some potential to tackle the most intriguing challenges of our time. His success for example in the previous #TegetaEscrow scandle was not by virtual of himself alone rather by the input and contribution from PAC team, members of opposition including Chadema and the support from some of the CCM MPs who have realized that change is inevitable and have accepted to adapt to the direction of the wind. His contribution in politics is still important but in my view it will be much more pronounceable within the confines of Chadema, his political birthplace. Many Tanzanians who want change have cultivated their trust on Chadema not only because Zitto was in there but the sum total of all youthful and promising cadres and the consistent message of change. Politicians have to learn to live with their differences. Starting a new political party is not a panacea to addressing differences of individual party members as the law of divergence tells that humans are different, that there aren’t two humans who perfectly resemble in everything. To me that is Political Entrepreneurship and not health for our young democracy. We expected Chadema to exercise maturity in accommodating each other and especially in addressing those issues Zitto and the rest are complaining about, we too expected Zitto to weigh his ambitions at this material time and exercise wisdom of timing and exploit the advantages of the LAW OF CONCENTRATION.

Aliyewahi kuwa mpiganaji wa mstituni, Rais maskini kuliko marais wote duniani: Rais wa Uruguay ndugu Mujica aachia madaraka

March 3, 2015 § 1 Comment

Imechapishwa: March 01, 2015 12:36

Imeandikwa mwanzo na Reuters/Andres Stapff

kutafsiriwa na kadulyu.wordpress.com March 2, 2015

Mujica 1

Rais wa Uruguay, Jose Mujica, almaarufu ‘Pepe’, ambaye aliwahi kuwa mpiganaji wa msituni, ambaye muda wote amekuwa akiishi katika shamba lake amekuwa akitoa sehemu ya mshahara wake kwenye shirika la misaada, sasa ameachia madaraka baada ya kutawala miaka mitano, amekamilisha muhula wake akiwa mmoja wa viongozi maarufu sana duniani.

Mujica, (79), anaondoka madarakani akiwa na ukubali wa asilimia 65 ya watu wa Uruguay. Ameheshimu katiba inayomzuia kugombea vipindi vinavyofuatana.

Yeye anasema, ‘Nilipoanza kuwa rais nilijaa nadharia, lakini baadaye ukweli uligonga’, alisika akisema alipohojiwa gazeti la wiki hii la AFP.

Baadhi humwita “Rais maskini kuliko wote duniani”. Wengine, “Rais ambaye kila nchi wengependa wawe naye”. Lakini Mujica husema, “Bado kuna mengi ya kufanya” na ana matumaini kwamba serikali ijayo, itayoongozwa na Ndugu Tabare Vasquez (Ambaye kachaguliwa kwa mara ya pili Novemba mwaka jana) atakuwa, “bora kuliko mimi na atakuwa na mafanikio makubwa

Mujica amefanikiwa kuiweka Uruguay katika ramani ya dunia. Amefanikiwa kuibadili nchi ya wafugaji ya watu milioni 3.4 kuwa nchi inayouza nishati nje, Brazili ikiwa nchi inayoongoza kama soko lao (ikifuatiwa na China, Argentina, Venezuela na Marekani).

Uruguay's President Jose Mujica speaks beside his dog  Manuela during an interview with Reuters in his farm in the outskirts of Montevideo

Uchumi wa Uruguay wa Dola za kimarekani billion 55 umekuwa ukikua kwa asilimia 5.7 kila mwaka kuanzia mwaka 2005, kwa mujibu wa benki ya dunia. Deni la Uruguay likilinganishwa na pato la taifa (yaani uwiano kati ya deni na patoa la taifa – debt-to-GDP ratio) limekuwa likipungua kutoka asilimia 100 mwaka 2003 hadi asilimia 60 mwaka 2014. Kwa muda huo pia gharama za deni hilo zimepungua pia ikiwemo matumizi ya dola kutoka asilimia 80 mwaka 2002 hadi asilimia 50 mwaka 2014. Takwimu hizi bila shaka zinadhirisha taifa linaloongozwa na mtu makini.

Mwenyewe anasema, “Tumekuwa na miaka chanya ya usawa. Miaka kumi iliyopita Waurguay asilimia 39 waliishi chini ya kiwango cha umaskini; tumeshusha kiwango hicho hadi asilimia 11 tu na tumepunguza watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri kutoka aslimia 5 hadi 0.5”.

Baada ya kushindwa kwa jitihada za nchi za Amerika ya kusini kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya, nchi hii ya Amerika ya kusini ikawa nchi ya kwanza duniani kuhalalisha matumizi ya bangi, Mujica alisimamia hoja kwamba biashara ya madawa ya kulevya ni hatari zaidi ya bangi yenyewe. Huo ndio ulikuwa msimamo wake sie kwetu hapa bangi ng’o. Japo nasikia kuna watu wametajirika sana na bangi hapa kwetu Tanzania.

Kwa kweli ni miongoni mwa marais wenye upeo mkubwa katika eneo la Amerika ya Kusini. Ingawa Mujica amefanya mambo mengine ambayo hayakubaliki katika jamii na imani zetu kama kuhalalisha ndoa za jinsia moja, amekuwa rais wa kwanza kuwakubali wazuiwa wa Guantanamo Bay kule Cuba. Wazuiwa wa Marekani 6 ambao walikuwa hawajashitakiwa kwa kosa lolote walikaribishwa Uruguay kama wakimbizi. Hawa walikuwa Wasyria wanne, Mpalestina na Mtunisia. Ingawaweje waliruhusiwa kuachiwa tanu mwaka 2009, Marekani haikuwaachia hadi pale rais wa Uruguay alipokubali kuwapokea.

Uruguay's President Jose Mujica waves to the people after receiving the Uruguayan flag on the last working day of his term in Montevideo

(Reuters/Andres Stapff)

Ndani ya mafanikio hayo na utata katika maamuzi hasa ya mambo ya kijamii, tukumbuke kwamba rais Mujica alikuwa kiongozi wa wapiganaji waasi wa msituni wa mrengo wa kushoto, alifungwa miaka 13 jela wakati wa utawala wa kidikteta na kijeshi. Alihimili mateso na miezi mingi ya kuwekwa upweke. Lakini pamoja na yote Mujica anasema hajutii muda wake gerezani bali anaamini ulimsaidia kujenga tabia yake. Wengi leo ugumu tunaulaani japo wakati mwingi hutusaidia kutujenga. Raha maisha yote ya ujana, kula kulala havijengi vinaharibu.

Ukarimu wa Rais Mujica unaongea mengi na makubwa: Alikataa kuhamia Ikulu ya kifahari ya Uruguay ambapo ndio makao rasmi ya Rais, badala yake akachagua kuishi shambani mwake nje ya mji wa Montevideo akiwa na mkewe na mbwa kilema wa miguu mitatu. Pepe kama anavyojulikana alitoa asilimia 90 ya mshahara wake  mfuko wa misaada kwa maskini akisema hakuhitaji mshahara huo. Anaendesha gari aina ya Volkswagen Beetle ya mwaka 1987!

Mujica 4

Mwaka jana, Mujica alikataa ofa ya dola millioni moja kutoka kwa shehe wa kiarabu alotaka kununua gari lake. Pepe alikataa kuuza gari yake hiyo akisema, atawaudhi, ‘Marafiki zake ambao walichangia kuwanunulia hilo gari”

Alivyo mtu wa pekee kuna siku moja aliwahi kusimama na kumpa lifti kijana aitwaye Gerald aliyekuwa amesimama pembeni akiomba lifti. Aliposhushwa alishukura sana na kushangaa kupewa lift na rais wa nchi maana wote walimpita lakini yeye alisimama na kumsaidia.

Mwisho

Kiongozi bora ni yule anayemaindi mabadiliko chanya ya watu na nchi yake na si yule anayeangalia mabadiliko yake tu. Viongozi wengi wameshindwa kuleta mabadiliko katika nchi zetu kwa tamaa tu ya kutajirika utajiri ambao kiuhalisia hatuendi nao popote. Wakati huu watu wanapofikiria kuwa viongozi katika ngazi mbalimbali wajihoji nia hasa yao nini? Ni kusavaivu tu kwa sababu hawana namna nyingine ya kuishi ama wanajitoa kwa ajili ya nchi yao hata kama wao watakufa maskini lakini potelea mbali nchi isonge? Ufisadi ambao tumekuwa tukiushuhudia kwa viongozi wetu kila kukicha unatisha na hauleti matumaini ya ama muda mfupi au mrefu. Ni bahati mbaya sana hakuna mgombea wa urais katika wale waloonyesha nia anayeyaona haya zaidi ya kujenga mfumo wa kulindana. Nani atatoka kama Mujica wa Uruguay?

Fanya mabadiliko katika eneo lako unalolimudu (Make change within your sphere of influence)

March 3, 2015 § Leave a comment

Leo nimeenda asubuhi kwenye duka moja kubwa wenyewe mwaita supa maketi, mie mpenzi wa karanga na korosho. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikienda pale kununua hizo njugu (nuts). Muda fulani uliopita niliacha baada ya kugundua ubora wa zile karanga umebadilika yaani umeshuka. Lakini basi kila wakati hupita kuona kama kuna mabadiliko chanya ya ubora wa hizo karanga. Ajabu kila ninazozikuta ni mbaya zaidi kwa maana zimeungua zaidi, uchafu mwingi na zilizooza zinaonekana wazi zaidi.

Nilipokuwa hapo leo kwa hiyo shelf nikatafakari nikaona kuwa hili jambo la kuwa naumia tu na kuondoka haifai ngoja nijaribu kuvuka kidogo msitari wa upole wangu. Mwezenu nilikuwa nimetokelezea kipamba pia na kamkia ka shingoni, si mwajua tena sie watu wa mara moja kwa mwezi! Ukiniona waweza fikiria ni miongoni mwa wale wala mboga za milioni kumi nini! hahahah!

Basi nikachukua pakiti ya karanga, nikajivalisha sura ya mamlaka kidogo (baada ya kukumbuka ule usemi mfalme sijui ni mteja ooh hapana, ‘Mteja ni mfalme) nikauliza mfanyakazi mmoja wa hapo dukani, nani mkuu wa hapa? Kanionyesha jamaa mmoja ambaye naye alikuwa kaweka kipamba chake kuonyesha kweli ni mkuu pale. Nikamfuata yapata kama mita kumi hivi kutoka kwa ile shelf, mita kumi zilinipa muda wa kupanga hoja na kuzoea mwonekano wa kimamlaka niliouvaa muda mfupi. Nilimuuliza swali moja tu, ‘Ubora wa hizi karanga unalingana na hadhi na heshima ya hili duka?’, swali lililofuata, ‘Hili duka kubwa mna mpango gani wa kusaidia wajasiriamali kuinua ubora wa bidhaa zao?’

Yule mkuu nikaona kashtuka na kupata woga hivi. Nikarekebisha kidogo uimla niliomwingia nao. Akachukua ile bidhaa tukafuatana naye kwenye ile shelf, kila akiokota pakiti tatizo ni lilelile. Ndipo aliponigeukia na kuniomba radhi sana. Na kushangaa eti kupata mteja mkweli na jasiri wa kusema kisichomfurahisha. Na akakiri kwamba ni kweli hiyo bidhaa haiendi siku hizi. Mwisho niliona wanaiondoa bidhaa yote kwa shelf, wakampigia muuzaji wa hiyo bidhaa aje kuichukua mara moja.

Nikawaambia ili kuleta nidhamu katika ubora wa bidhaa zetu hapa nchini ni vizuri wafanyabiashara wa kati wawe wanaelekeza wajasiriamali wetu kuweka na kuheshimu viwango fulani vya ubora. Hii itatusaidia kuinua ubora wa bidhaa zetu hata zionekane zinafaa kuuzwa nje pia. Kwa nini isiwezekane? Kitu kingine nikajifunza kumbe wote tungechukua hatua katika mdura wetu wa mvuto (our sphere of influence) tunaweza kuleta mabadiliko. Na ujumla wa mabadiliko madogo madogo ya sisi wanyonge yatajijenga na kuwa mabadiliko makubwa tena ya kudumu (sustainable changes). Naitoa hii stori ya kweli kwa wote wapenda mabadiliko.

Where Am I?

You are currently viewing the archives for March, 2015 at kadulyu.