Baadhi ya Walimu ni Watoro, wakija hawafundishi na hasa wale wa Kiingereza na Hesabu
July 16, 2012 § Leave a comment
Hebu jisommee hii ripoti ya listening Dar uone ncha tu ya barafu iliyojitokeza juu ya bahari ya elimu wakati chini kuna mwamba mkubwa wa barafu unaoweza kupasua meli ya maisha ya Watanzania.
Tuna tatizo kubwa kwenye mfumo mzima wa elimu. Vitabu, waalimu, vifaa vya kufundishia n.k. Mimi na wewe tufanyeje? Nadhani tuanzie majumbani kwetu na watoto wetu. Waalimu wanalalamika kwa miaka mingi sasa, siasa zimetawala mtindo mmoja katika kushughulikia matatizo yao. Ripoti inaonyesha hata wakienda darasani hawafundishi, tutamlazimisha ng’ombe kunywa maji kweli?
Ni kweli serikali imeshindwa au sisi wananchi ndio tumeshindwa halafu tunaisingizia serikali. Nani wa kuwajibika? Mlipa kodi au mlipwa kodi? Hii ripoti ni ya Dar tu, pale wakubwa wanapokaa, vije kule mbali?
Kuna maneno! Haya pitia.
R10 education ENG-Teachers absenteeism
Leave a Reply